Amesema Qur’ani Tukufu imeibua ustaarabu ambao umewawezesha wanadamu kuishi pamoja kwa amani. "Qur’ani Tukufu inaweza kuchangia katika kutuwezesha kufahamu maana ya maisha katika utamaduni wa sasa wa kidijitali,” amesema Sheikh Hajji.
Mwanazuoni huyo kutoka Morocco amesema kuwa, Qur’ani Tukufu inawataka Waislamu watafakari na iwapo agizo hilo litafuatwa basi Waislamu katika nchi za Magharibi wanaweza kuboresha uhusiano wao na jamii wanamoishi.
Kikao hicho kilimalizika kwa kikao cha qiraa ya Qur’ani Tukufu kilichowajumuisha wasomaji 14 kutoka nchi mbali mbali za Ulaya.
3464517