Darsa za kuhifadhi Qur'ani zimenza Jumanne katika kategoria tatu na pia kuna darsa maalumu za watoto ambapo wanafunzi wamhudhuria ana kwa ana na waalimu wao.
Dkt. Abdel Moneim Fuad, msimamisi wa shughuli za kielimu katika Kituo cha Kiislamu cha Al Azhar amesema vikao vya kuhifadhi Qurani vitafanyika kama ilivyopangwa.
Aidha amesema watalenga kuwavutia wanafunzi sasa baada ya vizuizi vya COVID-19 kuondolewa.
Hivi karibuni Wizara ya Wakfu nchini Misri imetangaza kuwa darsa za kuhifadhi Qur'ani ndani ya misikiti kwa kuhudhuria ana kwa ana waalimu na wanafunzi zitaanza tena kote katika nchi hiyo.
Wazri wa Wakfu Sheikh Mohamad Mokhtar Gomaa amesema suhula za kisasa zitatumika darasani kuhu wanaoshiriki wakitakiwa kuzingatia sheria za kiafya za kuzuia kuenea COVID-19. Amesema misikiti yote itatenga maeneo maalumu ya kufundisha Qur'anikwa watoto kwa sharti kuwa suhula zinazohitajika zinanunuliwa.